Search This Blog
Thursday, 12 January 2017
MTUMISHI:LIKIZO YA MARADHI.
60.-(1) Taasisi italazimika kutafuta taarifa za mtumishi
aliyekuwa hajahudhuria kazini siku tano mfululizo na ikigundua
kuwa mtumishi huyo ni mgonjwa taasisi ifanye utaratibu wa
kumpatia matibabu.
(2) Mtumishi wa umma atakapopata maradhi
atastahiki likizo ya maradhi baada ya kupata idhini ya Daktari
wa Serikali kwa muda usiozidi siku 60 za kazi kwa mwaka
mmoja kwa malipo ya mshahara kamili bila ya kuathiri likizo
ya kawaida ya mtumishi huyo.
(3) Iwapo baada ya siku 60 kumalizika itaonekana
bado mtumishi anahitaji muda zaidi wa kupumzika kutokana
na hali mbaya ya afya yake, Daktari wa Serikali anaweza
kuidhinisha kwamba mtumishi anayehusika apewe
mapumziko mengine ya muda usiozidi siku 60 kwa malipo
ya mshahara kamili ambapo zitakatwa katika likizo yake ya
kawaida.
(4) Ikiwa baada ya kutolewa siku 120 za mapumziko
kutokana na maradhi kwa mujibu wa kanuni ndogo (2) ya
kanuni hii, mtumishi atakuwa bado hajapata nafuu ya
kumuwezesha kuendelea na kazi, atastahiki kufanyiwa
uchunguzi wa afya yake na Bodi ya Uchunguzi wa Afya za
Watumishi, kufuatana na mapendekezo ya Bodi hiyo, mtumishi
atapewa likizo ndefu ya maradhi ambayo haitopindukia siku
180 kwa malipo ya mshahara kamili. Likizo hii itolewe pale
itakapoonekana kuwa upo uwezekano wa mtumishi
anayehusika kupata nafuu katika muda huo, na kwamba nusu
ya likizo ndefu ya siku 180 za mwanzo italipwa kutokana na
likizo yake ya kawaida.
(5) Mtumishi aliye katika likizo ndefu ya maradhi
atapaswa kuangaliwa afya yake na Daktari wa Serikali
angalau mara moja kwa mwezi na pale atakapoonekana
Likizo ya
Maradhi.
86
amepata nafuu kiasi cha kuweza kuendelea na kazi atapaswa
kuendelea na kazi tarehe ambayo Daktari ataidhinisha hata
kama muda wake wa likizo ya maradhi haujamalizika.
(6) Mtumishi hatostahiki kuchuma likizo katika
kipindi cha likizo ndefu ya ugonjwa.
(7) Ikiwa hata baada ya likizo ndefu ya ugonjwa ya
siku 300 kwa malipo ya mshahara kamili mtumishi atakuwa
hajapata nafuu kiasi ya kuendelea na kazi anaweza iwapo
Daktari wa Serikali ataona kuwa kuna uwezekano wa
mtumishi anaehusika kupata nafuu kiasi cha kumuezesha
kuendelea na kazi, kuomba likizo bila ya malipo kwa muda
usiopungua miezi sita.
(8) Ikiwa hata baada ya kumalizika muda uliotajwa
hapo juu wa likizo ya maradhi, mtumishi anayehusika atakuwa
bado anaendelea kuumwa kiasi ya kutozimudu kazi zake,
mtumishi huyo hatostahiki muda wowote zaidi wa likizo ya
maradhi. Inapotokezea hali hiyo Katibu Mkuu au Mkuu wa
Taasisi atapaswa kuchukua hatua za kuitaka Bodi ya
Uchunguzi wa Afya za Watumishi iidhinishe mtumishi huyo
kustaafishwa kwa sababu ya maradhi.
(9) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni hizi, Mtumishi
aliyekuwemo katika kipindi cha majaribio anastahiki kupata
likizo ya maradhi.
(10) Ni jukumu la Katibu Mkuu au Mkuu wa Taasisi
kufuatilia taarifa za ugonjwa za mtumishi aliyekuwepo katika
likizo ya maradhi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment