Search This Blog
Thursday, 12 January 2017
LIKIZO YA UZAZI:WATUMISHI WA KIKE
61.-(1) Mtumishi wa umma anapojifungua atastahiki
likizo ya uzazi ya miezi mitatu kwa siku za kalenda.
Likizo ya
Uzazi.
87
(2) Likizo ya uzazi ya miezi mitatu itatolewa mara
moja kila baada ya miaka miwili na miezi tisa kwa watumishi
wanawake waliojifungua ambao wamo katika masharti ya
kudumu. Likizo hiyo haitaathiri likizo ya kawaida ya mwaka
ya mtumishi.
(3) Pindipo mtumishi wa kike atajifungua kabla ya
kutimiza muda uliotajwa chini ya kanuni ndogo (2) ya Kanuni
hii, atastahiki kupata mapumziko ya wiki sita za kalenda.
(4) Taarifa ya uzazi itatolewa na Mtumishi
aliyejifungua au mtu wake wa karibu kwa Katibu Mkuu au
Mkuu wa Taasisi kwa ajili ya kustahiki likizo ya uzazi ya
mtumishi huyo, taarifa hiyo lazima iambatanishwe na
kitambulisho cha kuzaliwa kwa mtoto kitakachotolewa
hospitali, Sheha au Kiongozi wa Mtaa au Kijiji.
(5) Itakapotokea mtumishi amejifungua mapacha
kipindi cha likizo kitaongezwa mpaka siku mia moja.
(6) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni hizi,
itakapotokea kuharibika kwa mimba au kufa kwa mtoto,
mtumishi huyo atapewa likizo ya wiki sita kutoka tarehe ya
kujifungua au kuharibika kwa mimba.
(7) Mtumishi ambaye likizo yake imekatishwa kwa
sababu ya kifo cha mtoto mchanga, akipata ujauzito kabla
ya kutimiza miaka miwili na miezi tisa kuanzia tarehe ya
kujifungua au kuharibika kwa mimba, mtumishi huyo atastahiki
likizo kama ilivyoelezwa katika kanuni ndogo (1) ya kanuni
hii.
(8) Hakuna mtumishi atakayefukuzwa, kuhamishwa
au kuachishwa kazi kwasababu za ujauzito au kujifungua.
88
(9) Mtumishi atakayejifungua atapewa saa moja ya
kunyonyesha kwa kila siku kwa kipindi cha miaka miwili.
Mtumishi huyo atachagua aidha kuitumia nafasi hiyo asubuhi
kabla ya kuja kazini au mchana saa moja kabla ya muda wa
kuondoka kazini.
(10) Mtumishi wa kike mjamzito na aliyejifungua
atahudhuria kliniki kwa mujibu wa maelekezo ya Daktari wa
Serikali na mahudhurio hayo hayatoathiri malipo yake ya
mshahara na stahiki nyengine.
(11) Mtumishi wa umma atakaejifungua katika muda
wa majaribio hatostahiki likizo iliyoelezwa katika kanuni
ndogo (1) ya kanuni hii, isipokuwa atastahiki kupata
mapumziko ya wiki sita za kalenda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment