Search This Blog

Wednesday, 11 January 2017

Maambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI -Urinary tract infection)

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg8XZLg4B8xzZDpe2GPjCG6uY0smxKzelg01CUdpRfxCD48QR2nCKCLVmR9KID9HznSZCMKjhjYC2tTPTBfyxe1OAWAtop1MjQBBU2K-GrA2-XE2EaHF9AF-m28d9CzaHFIrLlPOtf-L8gv/s1600/
Maambukizi kwenye njia ya mkojo  (UTI ) ni maradhi  ambayo huathiri mfumo wa mkojo yaani  figo, mirija  ya mkojo pamoja  na kibofu  cha mkojo.

Maradhi  haya  husababisha  na vimelea wa aina  mbalimbali . Bacteria ndio husababisha  UTI mara nyingi  zaidi  kuliko  vimelea  wengine.  Hata  hivyo fangasi  pia huweza  kusababisha  maambukizi kwenye njia ya mkojo.
"Kibofu  cha mkojo ndicho  kiungo  ambacho  huathirika  zaidi. Bacteria  wanaweza  kusambaa  kutoka kwenye  kibofu  cha mkojo na kuathiri  sehemu  zingine  kwenye  mfumo  wa mkojo"
Vimelea  hawa  huweza  kuingia  kwenye njia ya mkojo kwa  njia  mbalimbali. Mojawapo ni kutoka kwenye njia ya  haja kubwa kwenda kwenye njia ya  mkojo hasa wakati wa  kutawaza. Hivyo  ni vyema kutawaza toka  mbele  kurudi  nyuma  ili kuepuka kuingiza  vimelea  kwenye  mrija wa mkojo. Wanawake  wako  katikahatari kubwa ya kupata  maambukizi kwa sababu mirija yao  ni mifupi  ukilinganisha na wanaume.

Pia  vimelea  hawa  huweza  kuenezwa wakati wa  tendo la ndoa,na pia  kutawaza kwa wanawake

Dalili za  UTI
Iwapo  unapata  dalili  hizi  ni dhahiri kuwa  unaweza kuwa  na UTI.
•Kuhisi  maumivu  kama  kuungua  wakati wa kukojoa
•Kuhisi  haja  ya kutaka  kukojoa  mara kwa mara na unapokwenda  unapata  mkojo  kiduchu.
•Kuhisi  maumivu  chini ya tumbo  na hata  mgongoni
•kupata  mkojo wenye  rangi au damu
•Uchovu
•Kuhisi  homa  au baridi

Vipimo
Vipimo  hutolewa  katika  mkojo.  Mkojo unaweza  kufanyiwa  uchunguzi wa moja kwa moja  au kuoteshwa kwa siku kadhaa.

Matibabu
Maambukizi ya kibofu cha  mkojo  hayana madhara  makubwa  kama yakitibiwa haraka. Mgonjwa huweza  kuandikiwa dawa  za  kunywa  au sindano  kutegemea hali ya mgonjwa.

Maambukizi  ya figo  huweza  kusababisha mgonjwa kupata  maradhi sugu ya figo  na hivyo  figo  kushindwa  kufanya  kazi vizuri.
Pia bacteria  huweza  kuenea katika sehemu  mbalimbali za mwili hivyo kusababisha  madhara zaidi  na hata  kifo.

Unashauriwa  kufanya  yafuatayo ili kupunguza kupata  maambukizi  mara  kwa mara
•Hakikisha  unakunywa maji ya kutosha kila siku  angalau  lita 3
•Hakikisha  unakojoa  unapohisi haja.  Epuka  kubana  mkojo.
•Kojoa  kila  baada ya  tendo la ndoa
•Nawa  kabla ya  kukutana  kimwili
•Tawaza  toka  mbele  kurudi nyuma kila  baada ya  haja  kubwa
•Kula  matunda na vyakula vya protein

No comments:

Post a Comment